MORINHO ATAAMUA MATOKEO YA MECHI YA LEO
![]() |
| Jose Morinho kocha wa Man U |
,
Usiku wa leo katika ligi kuu ya Uingereza "EPL" kutakuwa na mpambano mkali kati ya timu ya Manchester United au "mashetani wekundu" kama wanavyojiita ambao watakaribishwa na Liverpool katika jiji la Liverpool uwanja wa Anfield.
Hii ni mechi ya kihistoria na ni mechi inayobeba hisia kubwa kwa wapenzi na mashabiki wa soka hususani walio nchini Uingereza kama siyo duniani kwa ujumla.
Hii ni mechi ya watani wa jadi licha ya kwamba kila timu ina mtani wake ambaye anatengeneza naye mchezo uitwao "derby" ambapo Manchester United watani wao ni Manchester City huku Liverpool watani wao ni Everton.
Lakini mechi kati ya Liverpool na Manchester United inabeba hisia kubwa kutokana na historia ya majiji hayo mawili nchini humo. Kabla jiji la Manchester halijawa na miundo mbinu mizuri ya kiuchumi wakazi wake haswa wafanyabiashara walitegemea bandari na miundo mbinu mingine kutoka ktk jiji la Liverpool. Baada ya Manchester kujenga bandari na kuimarisha jiji lao walianza kujitegemea na hilo ndilo lililoanzisha uhasama kati yao kiasi cha kuhamishia uhasama huo kwenye mchezo wa mpira na kusababisha timu zao kuwa na upinzani wa jadi.Mchezo wa leo unakuja huku kukiwa na maneno mengi kuhusiana na mwamuzi wa mchezo huo ambao unazikutanisha timu hizo zikiwa kwenye viwango tofauti toka ligi imeanza. Liverpool wanaolilia taji la 19 la ligi hiyo baada ya miongo zaidi ya miwili toka walipofanya hivyo.
Manchester United nao wanataka kurejea katika zama zao baada ya kutofanya vizuri kwa zaidi ya misimu zaidi ya minne toka alipoondoka kocha maarufu wa klabu hiyo Sir Alex Ferguson.
![]() |
| Jurgen Klopp kocha wa timu ya Liverpool |
Endapo Jose Morinho ataamua kumtumia Paul Pogba katika eneo la kiungo cha kukaba samba na ama Maruan Fellain au Carrick au Herera basi Manchester United watakuwa na tatizo kubwa sana kwenye kuzuia kasi wachezaji wa Liverpool wenye kasi kubwa kama Fellipe Cotinho.Sadio Mane pamoja na Roberto Firmino ambao wote wana kasi kubwa hasa wanapovuka mstari wa kati ya uwanja kuelekea eneo la tatu la timu pinzani.
Tunatazamia mchezo wa kukata na shoka pale Anfield mcheo ambao naamini matokeo yake yataamuliwa na mbinu za makocha wa pande zote mbili


Tusubiri game saa nne usiku.
ReplyDeleteKikubwa mimi km mshabiki wa Arsenal naomba timu hizo zitoke sare tu au Man United afe
ReplyDeleteHaina namna Liverpool chapa hao wazee wa Media na Klopp endeleza ufalme wako kwa Mourinho
ReplyDelete