POLISI:TAARIFA ZA KIFO CHA MWANAMASUMBWI THOMAS MASHALI ZINATOLEWA KESHO
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema kuwa wanaendelea na upelelezi kufuatia kuuawa kwa mwanamasumbwi Thomas Mashali na watatoa taarifa ya kifo hicho siku ya kesho Jumatano.
Akizungumza na waandshi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro alisema taarifa zilizopo kufuatia kifo cha bondia huyo ni za kufikirika na zinasemwa tu, hivyo Jumatano atatoa taarifa hiyo.
Kamishina Sirro alisema kuwa bondia huyo ni mtu mkubwa na hakuna mtu aliethibitisha kuwa ni mny'ang'anyi, hivyo mpaka sasa ni maneno ya mtaani tu.
Post a Comment