Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

WAKAZI WA MTAA WA SINZA D WALALAMIKIA KUTOPATA TAARIFA ZA MAPATO NA MATUMIZI KWA WAKATI


Na Mainda Marijani,Dar es Salaam.

WAKAZI  wa Mtaa wa Sinza D kata ya Sinza wilaya ya Ubungo Jijini Dar es Salaam wameulalamikia  uongozi wa mtaa huo kutokana na  kutotoa kwa wakati taarifa juu ya ufafanuzi wa  wa mapato na matumizi ya serikali ya mtaa huo.

Akizungumza na Tanganyika Fm mmoja wa wananchi hao bw. Christopher Osmond amesema baadhi ya wananchi katika eneo hilo wanashindwa kupata taarifa hizo kwa wakati muafaka kutokana na Utaratibu uliopo sasa ambao si mzuri katika kutoa taarifa za mapato na matumizi hivyo ameshauri uongozi wa mtaa  kuweeka utaratibu unaeleweeka.

“ Baadhi ya watu hawajui kusoma hatimaye hukosa kujua kinachoendelea katika maeneo wanayoishi  hivyo tunaomba serikali ya kata itusaidie kufafanua na kutoa taarifa kwa wakati,” alisema Osmond.

Naye katibu mtendaji  wa ofisi ya kata akizungumza kwa niaba ya Afisa mtendaji bi. Zawadi Ayubu alisema wao hupata taarifa kutoka serikali za kata na kuzifikisha manispaa na baada ya hapo taarifa hizo hubandikwa katika kuta za ofisi yao.

Hata hivyo ametoa wito kwa wakazi wa mtaa huo kuwa na utaratibu wa kuchangia huduma mbali mbali katika mtaa huo kwa lengo la kuhakikisha gurumdumu la maendeleo linasonga mbele.


Aidha ameongeza kuwa muitikio kwa wananchi ni mzuri na changamoto hazikosekani lakini kwa kiwango kikubwa wananchi hao wana uelewa wa kutosha juu ya masuala mbali mbali na kuwataka kushirikiana kikamilifu na uongozi ili kukabiliana na changamoto hizo. 

No comments

Powered by Blogger.