Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

WANANCHI WAASWA KUTOA TAARIFA WANAPOPATWA NA MADHARA YA DAWA.



Na Joseph Peter -MAELEZO

WANANCHI waaswa kutoa taarifa pale wanapohisi wamepata madhara ya dawa wanazozitumia ili kuirahisishia Wizara ya Afya kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuchukua hatua stahiki zidi ya watengenezaji wa dawa hizo ili zisiendelee kuwadhuru wananchi.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kwenye hafla ya uzinduzi wa mfumo wa kielektroniki wa utoaji wa taarifa za madhara ya dawa uliofanyika jijini Dar es salaam.

Waziri Ummy amesema kuwa wananchi wawe mstari wa mbele katika kutoa taarifa pindi wanapohisi kupatwa na madhara ya dawa wanazozitumia ili kuirahishia TFDA kuchukua hatua stahiki kutokana na taratibu na sheria zilizopo za kuondoa madawa feki nchini.

“Napenda kusisitiza kwa wananchi wote kutoa taarifa pale wanapohisi wamepata madhara ya dawa ili kuirahishia TFDA kuchukua hatua stahiki kutokana na utaratibu na sheria zilizowekwa” alisema Waziri Ummy.

No comments

Powered by Blogger.