Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

DSTV YAJA NA ZAWADI KWA WATEJA WAKE, JOTI KUIPAISHA TANZANIA



Lucas Mhavile "JOTI" balozi wa DStv Bomba


Na; Imani Kelvin Mbaga 
Kampuni ya MULTCHOICE Tanzania imeamua kutoa zawadi ya sikukuu kwa wateja wake kwa kupunguza bei katika kifurushi cha DStv bomba ikiwa ni pamoja na kuongeza chaneli nyingi zaidi kwenye kifurushi hicho.
Hayo yamebainishwa leo na meneja mwendeshaji wa kampuni hiyo, Ronald Shelukindo, akiongea na waandishi wa habari katika hoteli ya Serena wakati wa hafla ya kumtambulisha balozi mpya wa kampuni hiyo msanii wa vichekesho hapa nchini, Lucas Mhavile (Joti).

DStv ambao wapo katika mkakati wa kuboresha huduma zao hapa nchini, wametangaza punguzo la kifurushi cha DStv bomba ambacho hapo kabla kilikuwa kinalipiwa shilingi 23,500/- za kitanzania na sasa kitalipiwa shilingi 19,975 na bei hiyo inaanza leo tarehe 15 Novemba.
Ronald Shelukindo meneja mwendeshaji wa MULTICHOICE Tanzania

Pamoja na punguzo hilo MULTICHOICE pia walitangaza kuongezwa kwa chaneli mpya katika kifurushi hicho kama vile B4U Movies, SuperSport  4, Eva Plus, Supersport  12, na FoxLife.

Shelukindo pia alitanabaisha kuwa wateja wa kampuni  hiyo wataendelea kupata burudani ya matangazo ya mpira ya moja kwa moja “live” ya ligi ya England “EPL” ikiwa ni pamoja na michuano ya ligi ya Hispania “La Liga” kwa mara ya kwanza bila ya kusahau kombe la mataifa ya Afrika “AFCON” yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon  kuanzia January 2017.

Katika hatua nyingine kampuni hiyo imemtambulisha rasmi msanii wa vichekesho nchini Tanzania, Lucas Mhavile maarufu kama JOTI kwa jina la kisanii kuwa balozi wao katika kutambulisha na kutangaza kifurushi hicho cha DStv Bomba na atasaidia kutangaza kifurushi hicho.

Akiishukuru kampuni hiyo, JOTI alisema kuwa ni fahari kwake kufanya kazi na DStv hasa katika bidhaa inayowajali watu wa kawaida wenye kipato cha kawaida kama yeye na kwamba atafanya kazi hiyo kwa nguvu.

“nilifurahi sana nilipoambiwa kuwa natakiwa kuwa balozi wa DStv, na mimi ni msanii na hali yangu ni sawa na watu nitakaowatumikia katika jukumu langu hili, nashukuru kwamba na DStv wameamua kuwakumbuka watu wa kawida” Alisema JOTI.

No comments

Powered by Blogger.