Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

INIESTA AREJEA KUNOGESHA EL-CLASSICO

Andres Iniesta nahodha wa Barcelona

Na: Imani Kelvin Mbaga

Kiungo mahiri na nahodha ya klabu ya Barcelona, Andres Iniesta ambaye amekuwa nje ya dimba kwa muda mrefu, sasa anatarajiwa kuwa vizuri kuwavaa Real Madrid katika mechi kubwa maarufu El-classico.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu ya Barcelona, Iniesta anaendelea vizuri na mazoezi na kwamba atakuwemo katika kikosi kitakachokwaana na watani wao wa jadi Real Madrid wanaoongoza ligi ya Hispania kwa sasa La liga.

Iniesta hajaonekana dimbani kwa muda mrefu na pengo lake limekuwa likioneka kutokana na kukosekana kwa ubunifu katika eneo la kiungo.

Taarifa za kurejea kwake zimepokelewa kwa furaha kubwa na wapenzi wa klabu hiyo ulimwenguni kote, ambao wamekuwa katika wakati mgumu kutokana na namna wapinzani wao wanavyofanya vizuri.


No comments

Powered by Blogger.