MULTICHOICE TANZANIA YAWAPA MKONO WA SIKUKUU WATOTO YATIMA
| Mkurugenzi mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande akikbidhi msaaada wa vitu mbalimbali kwenye kituo cha watoto yatima cha Al-madina kilichopo Tandale |
Na: Imani Kelvin Mbaga, Dar es salaam.
Kampuni ya
Multchoice Tanzania imefanya ziara ya kijamii na kutoa msaada kwa kituo cha
watoto yatima cha Al-madina kilichopo Tandale, katika kipindi hiki cha kuelekea
mwishoni mwa mwaka na msimu wa sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya.
Mkurugenzi
mtendaji wa Multichoice Tanzania, Maharage Chande, akiambatana na wafanyakazi
pamoja na waandishi wa habari, walifika kituoni hapo saa 4:10 asubuhi na
kukabidhi zawadi mbalimbali zenye thamani ya shilingi milioni tano na
kupokelewa na mlezi wa kituo hicho Kuruthum Yusufu.
Akizungumza
wakati wa hafla fupi ya kukabidhi msaada huo, mkurugenzi huyo wa Multichoice
Tanzania, alisema wamekuwa na utaratibu wa kujihusisha na utoaji wa misaada
kwenye jamii hasa katika vituo vya watoto yatima kama cha Al-madina ili
kuimarisha mahusiano yaliyopo kati yao na jamii.
“Huu ni
utaratibu wetu wa kawaida, na kituo hiki ni moja kati ya vituo ambavyo tuna
mahusiano mazuri, nah ii siyo mara ya kwanza kwetu kufanya hivi hata mama
Kuruthum anafahamu hilo” Alisema mkurugenzi huyo.
“Tulikuja
hapa wakati wa sikukuu ya EID na kutoa masaada, lakini pia tumewahi kuwapatia
msaada wa cherehani za kushonea nguo kama namna ya kuwasaidia kujitegemea
badala ya kutegemea misaada” Aliongeza mkurugenzi.
Naye mlezi
wa kituo hicho, Kuruthum Yusufu alitoa shukrani zake kwa Multichoice Tanzania,
na kusema kuwa kampuni hiyo imekuwa msaada mkubwa kwao katika nyakati tofauti
tofauti, na aliomba wadau wengine kuwa na moyo wa kujitolea kama Multichoice
wanavyofanya.
Katika ziara
hiyo kampuni ya Multichoice ilitoa msaada wa vyakula, vinywaji, sabuni na sare zipatazo
hamsini za shule kwa watoto wanaosoma katika shule mbalimbali kutoka katika
kituo hicho chenye jumla ya watoto sitini wanaolelewa hapo.
| wafanya kazi wa Multichoice wakibeba misaada kabla ya kuikabidhi kwenye kituo cha watoto yatima cha Al-Madina |
| Baadhi ya misaada iliyotolewa na kampuni ya Multichoice Tanzania kwa kituo cha watoto yatima cha Al-Madina Tandale kwa Tumbo |
| Mkurugenzi wa Multchoice Tanzania, Maharage Chande akikagua kazi za mikono zilizofanywa na watoto yatima wa kituo cha AL-Madina |
Post a Comment