Swali
kutoka kwangu…
JPM YANINI
KULEA BATA KWENYE BANDA LA KUKU?
Na:Nsajigwa Gostance Mwalugaja
Binafsi
huwa najiona kama shilingi yenye thamani na bahati kubwa hapa
Tanzania,ikumbukwe sifa ya kubwa ya shilingi ni kuwa na pande mbili zenye
kunakshi tamaduni na historia ya nchi husika.
Katika
makuzi yangu nimebahatika kupata malezi kutoka kwenye familia ya mfugaji, hivyo
kunipa fursa kujua aina na tamaduni za mifugo mbalimbali, hususani ngombe, mbuzi,
kuku na bata wa aina mbalimbali, kwa faida ya msomaji kuchi ni aina ya kuku wengi wakiasisi uasilia wake na mkoa wa
mwanza, tabia nzuri ya kuchi ni kwamba anaumbo kubwa na nyama nyingi wafugaji
wengi humfuga kwa madhumuni ya kula nyama na sio biashara kwa kuwa kuchi dume
hana tabia ya kupanda mara kwa mara, hii tabia humtofautusha na kuku aina ya
kishingo ambae tetea lake hutaga mayai wastani na jogoo aina ya kishingo hupenda
sana kupanda matetea wakati wowote.
vivyo
hivyo,kuna aina tofauti za bata na tabia tofauti tofauti,pamoja na utofauti
uliopo katika aina zao na tabia zao,bata na kuku kila mmoja huwa na tabia moja
ambazo huwatofautisha pasipo kuangalia aina ya zao,malezi bata wote hufanana
katika malezi ya watoto wao na kuku wote hufanana katika malezi yao .
Bata
siku zote hupenda kutanguliza watoto wake katika safari zake katika makuzi yote
ya watoto wake lakini kuku yeye hutangulia mbele na kumwaacha vifaranga vyake
nyuma,kinadhali binadamu hutafsri malezi ya bata kuwa huwaweka watoto mbele ili
kuona adui yeyote wa watoto wake lakini kwa upande wa pili malezi ya kuku
hutafsiliwa kuwa hupenda kuhakiki mapito ya watoto wake kabla hawajapita lazima
ahakikishe kuwa sehemu hiyo ni salama.
Ufugaji
imekuwa ni shughuli rasmi ya kiuchumi na kijamii katika jamii ya
kitanzania,binafsi nasema haya kwa kuwa nimebahatika kuwepo katika awamu
tano za uongozi katika taifa langu la
Tanzania,nina maana awamu ya kwanza ya mwl. Julius Kambarage Nyerere, awamu ya
pili ya mh:alhaji Ally Hassan Mwinyi,awamu ya tatu ya mh: Benjamin wiliam
Mkapa, awamu ya nne ya Mh: Jakaya Mrisho Kikwete na awamu ya sasa awamu ya tano
ya mh:John joseph pombe magufuli, Katika awamu zote hizi shughuli ya ufugaji
imekuwa na mchamgo wa kipekee katika malezi na maendeleo ya kila siku ya
watanzania
Katika
jamii yetu ya kitanzanzia ,tumekuwa tukiendesha maisha yetu kwa malezi tofauti
tofauti ambayo saa nyingine ni vigumu kutofautisha na makuzi ya vifaranga vya
kuku na bata,nikiwa kama mwana jamii nimekuwa nashuhudia mambo mengi tofauti
tofauti na imenichukuwa muda kutafakari mwisho wa siku najikuta katikakati ya
maswali,kati ya maswali mengi nabaki na swali moja kuu,ya nini kulea bata kwenye banda
la kuku?maana mambo yamekwa yakiingiliana katika Nyanja zote za
kisiasa,kijamii na kiuchumi pia.
Tarehe
14 october kila mwaka taifa la Tanzania huwa tunahadhimisha kifo cha baba wa
taifa la Tanzania mwl.Nyerere,natumia mapumziko haya kumuombea kwa mwenyezi
mungu amlaze mahala pema peponi lakini pia natumia mapumziko ya maadhimisho ya
miaka 17 tangu kifo cha mwl.Nyerere kutafakari baadhi ya mambo aliyoyaasisi
moja kati ya mengi mwenge wa uhuru, ambapo siku ya tarehe 14 october mwenge wa
uhuru huzimwa.
Tarehe
12 october 2016 rais wa jamhuri ya muungano alifuta safari za maafisa wa
serikali waliokuwa wanatakiwa kuudhulia sherehe za kuzimwa mwenge wa uhuru huko
mkoani simiu, rais aliagiza maafisa wote waliochukua fedha za safari
kuzirudisha na fedha hizo zipelekwe mwenye miradi ya maendeleo.
Hatua
ya rais magufuli kufuta safari za maafisa wa serikali kuudhulia sherehe za
kuzimwa kwa mwenge wa uhuru, ni hatua ya kizalendo ambayo binafsi naunga mkono
kwa asilimia nyingi sana, ni moyo wenye uthubutu pekee utakaothubutu kutoa
agizo ambalo kwa namna yoyote agizo hilo linakwenda kuwakwaza wanufaika, kwa
namna pekee rais alijaribu kuangalia masirahi yalio ya wengi
Hongera sana rais wane john pombe joseph magufuli, abagunana
bhako batamanile echo olelogwa?
Ikumbukwe
tangu kuapishwa kwa rais wa awamu ya tano, imekuwa wazi kuwa rais magufuli ni
mtu makini sana linapokuja suala la matumizi ya fedha za serikali mara kadhaa
amekuwa akitembelea maofisi ya serikali kuhakiki utendaji wa wafanyakazi na
matumizi ya mali za umma, hii ni kuhakikisha fedha ya serikali inayopatikana
kutokana na kodi ya watanzania inatumika vizuri.
Kumbukumbu
zangu zinanionyesha kuwa sherehe za muungano zilifutwa mwanzoni wa mwaka huu na
fedha zilizotakiwa kufanikisha sherehe hizo ziliamriwa zipelekwe kwenye miradi
ya maendeleo.
hivi
ni nani asiekumbuka jinsi mh.rais alivyosimamia kwa nguvu zote suala la
wafanyakazi hewa kutoka katika kila idara ya serikali Kwa
akili ya kawaida kabisa inajulikana Rais john pombe magufuli hapendi matumizi ya
fedha za wananchi ovyo ovyo lakini kwa hatua ya watendaji wa serikali wakiwemo
wakuu wa mikoa kupokea fedha za safari za kwenda kuzima mwenge Napata wakati
mgumu kidogo kuelewa kama wanaelewa falsa ya kiongozi wao juu ya kubana
matumizi ya fedha za umma rais wane, abagunana bhako batamanile echo olelogwa? ilikuwaje wakapokea
fedha pasipo kujiuliza faida ya safari zao, wamekosa nini katika utendaji wao, wamekosa
kujua falsa ya rais wao, wamekosa mwongozo wa maamuzi yao, wamekosa moyo wa
uthubutu wa kushauriana na viongozi wao kabla hawajaamua kufanya jambo?
Naamini
hatua hii ya rais kuwaagiza warudishe fedha za serikali haitawapa uoga bali
ujasiri wa kufikili na kuchukua maamuzi sahihi baada ya kushirikisha viongozi
wao.
Hii
ipo wazi siku zote Bata hupenda kutanguliza watoto wake katika safari zake
katika makuzi yote ya watoto wake lakini kuku yeye hutangulia mbele na kuwaacha
vifaranga vyake nyuma, Napata wakati mgumu kubainisha rais wangu kipenzi una
malezi ya aina gani, maana wasaidizi wako nimeshindwa kuwaelewa kwa kushindwa
kukuelewa.
kwa
asilimia 95 umepunguza safari za nje na ndani za kwako binafsi kwa nia ya
kupunguza matumizi ya serikali, umeamua kupita kwanza wewe ili kuonyesha watumishi wa serikali mapito
yalio salama kwa awamu ya tano lakini hii tabia ya wasaidizi wako kuwa mbele
wakisubili mwongozo wa kiongozi wao,hii inanichanganya kuku au bata nani
anamfumo sahihi wa malezi.
Tatizo
ni nini katika hili?tatizo ni kufuga bata kwa malezi na tamaduni za kuku,au
tatizo ni nyumba za kufugia hazirandani na tabia za mifungo?
Rais wane, ya nini kusuga mbata mwi banda la ngoko?
Nawasilisha
0713390903
0766610061


Post a Comment