Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

tuseme hapana,yatosha matumizi ya madini risasi ………… NAJIPENDA,NAIPENDA FAMILIA YANGU,NAIPENDA JAMII YANGU

Na: Nsajigwa mwalugaja
Image result
shughuli za uchimbaji wa madini

Risasi ni aina ya madini chuma yanayopatikana sana katika tabaka juu la dunia na kusambazwa zaidi duniani na shughuli za kila siku za mwanadamu.
Madini risasi katika mwili wa mwadamu ni sumu yanayoshambulia zaidi katika eneo la ubongo wa mwanadamu na kupunguza uwezo wa kufikiri na kuamua jambo kiufasaha,madhara yake hukuwa mpaka kusababisha kifo.
Madini risasi yamekuwa na madhara kubwa sana kwa watoto walio chini ya miaka sita na kwa kiasi kikubwa hushambulia ubongo nakudhuru siha makuzi  ya viungo vya mtoto,watoto hupata madini risasi kwa njia kuu mbili
·         shughuli za upakaji rangi kwenye makazi/kuta za nyumba zetu na mwilini,kubandika stika mwilini
·         vumbi lililoambatana na madini risasi katika shughuli za ujenzi
·         mabaki ya mabetri mbali mbali
·         maji yaliopita katika mabomba yaliotengenezwa na madini ya kopa
·         kuziba meno yalioharibika kwa kutumia madini risasi
·         shughuli za madini

     Dalili za madhara ya madini risasi mwilini
·         maumivu ya sio ya kawaida mwilini
·         maumivu ya kichwa mara kwa mara
·         usingizi wa mara kwa mara
·         mwili kutokuwa vizuri
·         kukosa hamu ya kula mara kwa mara
·         shinikizo la damu
·         kupoteza kumbukumbu ovyovyo na kuwa na uelewa mdogo
·         anemia
·         tatizo la kusikia vizuri

Maadhimisho ya wiki ya kupinga matumizi ya madini Risasi
kuelekea wiki ya tarehe 23 mpaka 29  ya mwezi October naungana na jamii ya wanaharakati wa maendeleo ya jamii ktika kupinga matumizi ya madini risasi ambayo kwa kiasi kikubwa yamekuwa yakisambaza sumu mwilini pindi yanapofanikiwa kuingia katika mwili
Ni vizuri jamii ikafahamu sumu ni nini,katika Kiswahili rahisi kabisa SUMU ni kitu chochote kinachoweza kuharibu wa kiasi kidogo au kikubwa seli katika mwili wa mwanadamu au kuweza kudhuru muundo wa seli au kiumbe hai
sumu ina patika na sehemu kuu tatu
·         mboga
·         wanyama kama nyoka,nyuki n.k
·         madini(asenia/zebaki)
nimeanza makala hii kwa kutoa ufahamu dhidi ya madini risasi kwa kuangali chanzo kikuu katika uenezaji wa madini risasi lakini pia kuanisha viashiria vya kudhurika na matokeo ya madini risasi ili jamii iweze kutambua madini risasi
jinsi ya kujikinga na madhara ya madini ya Risasi
·         ni vema jamii ikajitahidi kuzuia vumbi la aina yoyote
·         katika maandalizi ya chakula ni vyema kuandaa lishe kwa kutumia maji baridi
·         ni vema kunawa mikono kabla na baada kula
·          kutenganisha shughuli za upakaji rangi na uwepo wa watoto na kupaka rangi zisizo na madini risasi
·         ni vema kuwapima watoto wingi wa madini chuma,hususani watoto walio chini ya miaka 2
·         kusimamia usafi wa watoto kila watokapo kucheza

kuelekea october23-29
Mimi na wewe ni jukumu letu kuwalinda watoto wetu dhidi ya matumizi ya risasi mwilini
nawasilisha
0713390903

No comments

Powered by Blogger.