Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

UEFA CHAMPIONZ LIGI - DIMBANI JUMANNE: RONALDO, NAPOLI WAWANIA REKODI, GUARDIOLA KUREJEA BARCA!

BAADA ya kupotea kwa Wiki 3, Mechi za Makundi ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, zinarejea tena kilingeni hapo Jumanne na Jumatano Usiku na mvuto ni kuona Cristiano Ronaldo akiwania kuweka Rekodi mpya ya Magoli wakati Napoli ikitarajia kuweka Historian a pia Pep Guardiola akitua Klabu yake ya zamani FC Barcelona.

Kwenye mojawapo ya Mechi za Jumanne, Cristiano Ronaldo anawania kuwa Mchezaji wa Kwanza kufunga Bao 100 katika Mashindano ya Klabu Ulaya.

Jumanne, Real Madrid itaongozwa na Ronaldo kucheza Mechi ya Kundi F dhidi ya Legia Warsaw Uwanjani Santiago Bernabeu na Staa, mwenye Bao 98 Ulaya, anahitaji Bao 2 tu kuweka Rekodi mpya.

Nayo Klabu ya Italy Napoli ipo kizingitini katika kuweka Rekodi mpya ya UCL ikiwa wataifunga Besiktas kwenye Mechi yao ya Kundi B ambayo itachezwa Jumatano huko Italy.

Ikiwa Napoli watashinda Mechi hiyo na Dynamo Kyiv kutoka Sare na Benfica katika Mechi nyingine ya Kundi B, basi Napoli watafuzu kutinga Raundi inayofuata ya Mtoano huku wakiwa na Mechi 3 mkononi na hiyo itakuwa Rekodi Mpya kwa kuwa Klabu ya Kwanza kufuzu hivyo.

Nae Meneja wa Manchester City, Pep Guardiola, ataiongoza UCL-GROUP-E-F17OKTTimu yake hapo Jumatano kutua Nou Camp kucheza na FC Barcelona ambako ndiko alijijengea Jina.

Akiwa na Barca kama Mchezaji, Guardiola alitwaa Ubingwa wa La Liga mara 6 na wa Ulaya mara 1 na alipokuwa Kocha Mkuu alizoa Makombe 14 yakiwemo Mawili ya UCL.

Mara ya mwisho kwa Guardiola kuiongoza Timu nyingine kucheza na Barca huko nou Camp ilikuwa Msimu wa 2014/15 alipokuwa na Bayern Munich na kuchapwa 3-0 kwenye Nusu Fainali ya UCL.


UEFA CHAMPIONZ LIGI

Ratiba:

Jumanne Oktoba 18

Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku

KUNDI E

Bayer Leverkusen v Tottenham            

CSKA v Monaco              

KUNDI F

Real Madrid v Legia Warsaw                

Sporting Lisbon v Borussia Dortmund            

KUNDI G

Club Brugge v FC Porto            

Leicester v FC Copenhagen        

KUNDI H

Dinamo Zagreb v Sevilla            

Lyon v Juventus              

Jumatano Oktoba 19

Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku

KUNDI A

Arsenal v Ludo Razgrad            

Paris St Germain v Basel            

KUNDI B

Dynamo Kiev v Benfica              

Napoli v Besiktas            

KUNDI C

Barcelona v Man City                

Celtic v Borussia Monchengladbach                

KUNDI D

Bayern Munich v PSV Eindhoven          

FC Rostov v Atletico Madrid                                    

TAREHE MUHIMU:

MECHI ZA MAKUNDI:

Mechi ya Kwanza: 13 na 14 Septemba

Mechi ya Pili: 27 na 28 Septemba

Mechi ya Tatu: 18 na 19 Oktoba

Mechi ya Nne: 1 na 2 Novemba

Mechi ya Sita: 22 na 23 Novemba

Mechi ya Sita: 6 na 7 Desemba

MECHI ZA MTOANO:

11–12/04/17: Robo Fainali, Mechi ya Kwanza

18–19/04/17: Robo Fainali, Mechi ya Pili

02–03/05/17: Nusu Fainali, Mechi ya Kwanza

09–10/05/17: Nusu Fainali, Mechi ya Pili

03/06/17: Fainali (National Stadium of Wales, Cardiff)


No comments

Powered by Blogger.