Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

DIRISHA DOGO KUFUNGULIWA KATIKATI YA NOVEMBA



Na Imani Kelvin Mbaga

Ligi kuu ya kandanda Tanzania bara “VPL” inatarajia kukamilisha mzunguko wa kwanza tar 12 Nov mwaka huu na kuruhusu milango ya dirisha dogo la usajili kuanza ili kuwapa fursa vilabu mbalimbali vinavyoshiriki ligi daraja la kwanza pamoja na ligi daraja la pili kufanya usajili wa wachezaji kuziba nafasi zilizopo na kuimarisha vikosi vyao.
Alfred Lucas msemaji wa TFF
Kwa mujibu wa taarifa ya shirikisho la soka nchini TFF zilizotolewa leo jijini Dar es salaam na msemaji wake Alfred Lucas zilisema kuwa dirisha dogo  la usajili nchini litadumu kwa mwezi  mmoja kuanzia tar 15 ya mwezi Novemba hadi tar 15 ya mwezi Desemba mwaka huu.
“tunaviasa vilabu vyote kulitumia vizuri dirisha dogo la usajili ili kuimarisha vikosi vyao, tena vifanye hivyo kwa umakini ili kuhakikisha kuwa wanapata wachezaji bora kuziba nafasi zilizopo kwenye vilabu vyao” Alisema Lucas
Wakati huohuo shirikisho limesema kuwa linaridhishwa na mwenendo wa ligi hiyo hadi sasa na kwamba watahakikisha mzunguko wa pili unakuwa bora usio na malalamiko mengi.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena kesho katika jumla ya viwanja sita
Majimaji – Ruvu Stars
Mbeya City- Young Africans
Ndanda-Tanzania Prisons
Ruvu Shooting-African Lyon
Stand U-Simba
Toto Africans-Azam fc
Bado Simba inaongoza ligi hiyo kwa pointi 32 huku wakifuatiwa na mahasimu wao Yanga ambao wana pointi 27.

No comments

Powered by Blogger.