Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

KESI YA "KESSY" BADO NI "KIZUNGUMKUTI"



Na: Imani Kelvin Mbaga


Hatima ya mchezaji Hassan  “kessy” Ramadhani  inatarajia kujulikana tar 3 Novemba  baada ya kikao cha mariadhiano kati ya Simba na Yanga chini ya msuluhishi  huru, kiongozi  wa zamani wa  kilichokuwa chama cha soka nchini “FAT”, Said El-Maamri.
Hassan "Kessy" Ramadhan
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo msemaji wa shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF) Alfred Lucas, alisema  baada ya kesi hiyo kuwasilishwa kwenye kamati ya sheria maadili na hadhi za wachezaji  iliamuliwa kuwa vilabu husika vikae na kujadiliana juu ya suala hilo chini ya msimamizi huru na kwamba tar iliyopangwa ilikuwa ni tar 29 mwezi uliopita.
Hata hivyo suala hilo halikumzungumzwa siku hiyo kutokana na udhuru aliokuwa nao mwanasheria wa klabu ya Yanga Alex Mgongolwa, hivyo iliamuliwa shauri hilo liendelee tar 3 ya mwezi huu.
Hata hivyo shirikisho limevitahadharisha vilabu hivyo kukubaliana na visipofanya hivyo basi litarudishwa kwenye kamati husika na kuamuliwa kwa mujibu wa sheria.
Hassan “Kessy” alisajiliwa na klabu ya Yanga akitokea kwa mahasimu wao wa jadi Simba Sc ya jijini Dar es salaam huku Yanga wakidai kuwa alikuwa mchezaji  huru jambo ambalo limekanushwa mara kadhaa na klabu yake ya zamani Simba.
Suala hilo lilifikishwa kwenye kamati ya ya sheria, maadili na hadhi za wachezaji ambako mchezaji aliruhusiwa kuendelea kucheza soka ili kulinda kipaji chake wakati suala lake likiwa linashughulikiwa na vilabu vyake.

No comments

Powered by Blogger.