Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

SERENGETI BOYS KWENDA KOREA MWEZI HUU



Na Imani Kelvin Mbaga

Timu ya Taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 Serengeti boys inatarajia kuingia kambini hivi karibunui ili kujiandaa na michuano ya kirafiki ya kimataifa itakayo fanyika Korea ya kusini kuanzia tar 9 mwezi huu.
Msemaji wa TFF Alfred Lucas
Shirikisho la soka nchini TFF limesema vijana hao wataendelea kutunzwa na kwamba ahadi ya Rais wa shirikisho hilo Jamali Malinzi kwa vijana hao kuendelea kuwa timu za taifa na kupewa msaada wowote watakaouhitaji ili kufikia malengo ya shirikisho
Msemaji wa TFF Alfred Lucas alisema kocha wa timu hiyo Bakari Shime Nyundo amewasili leo kutoka mkoa Tanga na kwamba kambi hiyo itaanza hivi karibuni kabla vijana hao hawajaondoka kuelekea huko Korea ya Kusini.
Lucas pia ameeleeza kuwa timu ya taifa ya wakubwa yaani Taifa Stars itaitwa hivi karibuni ili kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Zimbabwe utakaochezwa katika wiki ya shirikisho la soka ulimwenguni FIFA .
“Zimbabwe wameonyesha nia ya kucheza nasi katika wiki ya michezo ya FIFA na baada ya kutuandikia barua ya kuomba kucheza na timu yetu tumekubali ili tukifanya vizuri tuweze kupanda katika nafasi za ubora za msimamo wa FIFA” Alisema Lucas
Kutokana na mchezo huo kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Charles Boniface Mkwasa, anatarajiwa kuita kikosi chake siku yoyote ili kuingia kambini kujiandaa na mechi hiyo muhimu.  

No comments

Powered by Blogger.