ARSENAL USO KWA USO NA BAYERN ULAYA, MAN UNITED YATUPWA UFARANSA
na Imani Kelvin Mbaga
Timu ya
Arsenal ya England imejikuta ikiingia mdomoni mwa timu ya Bayern Munich ya
Ujerumani katika hatua ya mtoano ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya
kufuatia droo iliyochezeshwa leo katika mji wa Nyon
Arsenal
maarufu kama washika bunduki wa jiji la London wamejikuta wakifadhaishwa na
droo hiyo kutokana na juhudi kubwa waliyoifanya kumaliza wa kwanza katika hatua
ya makundi ili kuepuka kukutana na timu ngumu lakini juhudi hizo zimeishia
kukutana na Bayern Munich ambao wameshika nafasi ya pili.
Arsenal na
Bayern wamekutana mara sita katika miaka minne ambapo Bayern wamefunga jumla ya
magoli 10 huku Arsenal wakifunga jumla ya magoli 7 katika mechi zote
walizokutana kama inavyoonekana hapa chini.
2012-13 (16 BORA)
Arsenal 1-3 Bayern Munich
Bayern Munich 0-2 Arsenal
2013-14 (16 BORA)
Arsenal 0-2 Bayern Munich
Bayern Munich 1-1 Arsenal
2015-16 (MAKUNDI)
Arsenal 2-0 Bayern Munich
Bayern Munich 5-1
Arsenal
Droo ya kupanga nani acheze
na nani katika hatua ya mtoano huziweka timu zilizoongoza makundi yao katika
sehemu moja na zile zilizoshika nafasi ya pili katika hatua ya makundi huwekwa
pamoja ili kuepuka kuzikutanisha timu zilizoshika nafasi sawa katika makundi
yao.
Wakati huo
huo timu za Hispania zimeendelea kutawala soka la Ulaya baada ya kutajwa zaidi
katika droo ya upangaji wa mechi za mtoano za vilabu barani humo, zinazohusisha
michuano ya klabu bingwa na kombe la Uropa, ambapo nchi hiyo imeingiza timu 7
kati ya timu 48 kutoka mataifa yote.
Timu za
Hispania zilizofanikiwa kuingia katika hatua ya mtoano kutoka nchi hiyo ni
pamoja na mabingwa watetezi wa kombe la klabu Bingwa barani humo, Real Madrid,
Barcelona, Atletico Madrid na Sevilla katika ligi ya mabingwa, kwa upande wa
Uropa ni Athletic Bilbao, Celta de Vigo na Villa Really.
England
imefanikiwa kuingiza timu tano katika hatua hiyo, baada ya Arsenal, Leicester
City na Manchester City kusonga mbele katika klabu bingwa, wakati ambapo
Manchester United na Tottenham Hotspurs zikisonga katika michuano ya Uropa.
Hatua ya
mtoano ya michuano ya vilabu barani Ulaya inatarajiwa kuanza kuchezwa tar 14 na
15 mwezi Februari ambapo timu zote zilizo shika nafasi ya kwanza katika makundi
yao zitaanzia ugenini na kumalizia nyumbani kama inavyoonekana katika ratiba
kamili hapa chini
M anchester City vs Monaco
February 21 - Manchester
March 15 - Monaco
Real Madrid vs Napoli
February 15- Madrid
March 7 - Naples
Benfica vs Borussia Dortmund
February 14 - Lisbon
March 8 - Dortmund
Bayern Munich vs Arsenal
February 15 - Munich
March 7 - London
Porto vs Juventus
February 22 - Porto
March 14 - Turin
Bayer Leverkusen vs Atletico Madrid
February 21 - Leverkusen
March 15 - Madrid
Paris Saint Germain vs Barcelona
February 14 - Paris
March 8 - Barcelona
Sevilla vs Leicester City
February 22 - Seville
March 14 - Leicester
RATIBA YA MICHUANO YA MTOANO UROPA
|
|||||
Astra Giurgiu V KRC Genk
|
18:00
|
|
Athletic Bilbao V Apoel Nicosia
|
18:00
|
|
AZ Alkmaar V Lyon
|
18:00
|
|
Borussia Mönchengladbach V Fiorentina
|
18:00
|
|
Celta Vigo V Shaktar Donetsk
|
18:00
|
|
FC Rostov V Sparta Prague
|
18:00
|
|
FK Krasnodar V Fenerbahçe
|
18:00
|
|
Hapoel Be'er Sheva V Besiktas
|
18:00
|
|
KAA Gent V Tottenham Hotspur
|
18:00
|
|
Legia Warsaw V Ajax 18:00
|
||
Ludogorets Razgrad V FC Copenhagen
|
18:00
|
|
Manchester United V Saint-Étienne
|
18:00
|
|
Olympiakos V Osmanlispor
|
18:00
|
|
PAOK Salonika V FC Schalke 04
|
18:00
|
|
Villarreal V Roma
|
18:00
|

Post a Comment