ARSENAL WATINGA 16 BORA KWA STAILI HUKU PEREZ AKITUMA SALAMU KWA WENGER
Na: Imani Kelvin Mbaga
Washika
bunduki wa jiji la London, timu ya Arsenal jana walifanikiwa kutinga hatua ya
16 bora katika ligi ya mabingwa barani Ulaya kwa staili ya aina yake baada ya
kufanya kile walichoshindwa kufanya kwa miaka takribani mine iliyopita baada ya
ya kufanikiwa kuongoza kundi.
Jana
zilichezwa mechi za mwisho katika hatua ya makundi, ambapo makundi A, B, C na D yalimaliza michezo yao na kushuhudia
timu nane kutoka makundi hayo zikikata tiketi kucheza hatua ya 16 bora wakati
timu nne zikirudi kucheza EUROPA na timu nne kutupwa nje ya mashindano hayo
msimu huu.
Arsenal walifanikiwa kupata nafasi ya kuongoza kundi
A kwa kujikusanyia alama 14 mbele ya PSG
ya Ufaransa iliyomaliza na alama 12 katika kundi hilo. Arsenal walimaluizia
mchezo wao wa mwisho kwa ushindi wa 4-1 dhidi ya Fc Basel ya Uswizi huku PSG
wakiambulia sare ya 2-2 nyumbani dhidi ya Ludogorates.
Tangu mwaka
2005 Arsenal hawajawahi kumaliza hatua ya makundi bila kupoteza mchezo kama
ilivyotokea safari hii, na miaka mine iliyopita mashabiki wa Arsenal wamekuwa
wakililia angalau kuiona timu yao ikimaliza ya kwanza katika hatua ya makundi
ili kuepuka kukumbana na vigogo katika hatuia ya mtoano.
Naye
mchezaji aliyesajiliwa msimu huu kutoka Deportivo La Coruna, Lucaz Perez, alijiwekea
rekodi mpya baada ya kufunga mabao matatu yaani “hat trick” kailka mchezo huo,
na kuwa mchezaji wa sita wa Arsenal kufunga “hat trick” katika michuano hiyo
baada ya Thiery Henry, Niklas Bendtiner, Olivier Giroud, dan Wellbeck, Mesuit
Ozil nayeye Lucaz Perez.
Timu
zilizofanikiwa kusonga mbele baada ya mechi za jana za makundi hayo ni kundi A,
Arsenal na Psg, kundi B, Napoli na Benfica, kundi C, Barcelona na Manchester
City, kundi D, Atletico Madrid na Bayern Munich.
Leo timu
nyingine nane zinatarajiwa kujulikana baada ya michezo ya makundi E, F, G na H kuchezwa kasha UEFA watafanya droo
kujua nani atakutana na nani katika hatua hiyo ya 16 bora mwanzoni mwa mwaka
ujao.
![]() | |||||||||||
| Mlinda mlango wa Arsenal David Ospina akiokoa hatari langoni mwake katika wa mchezo wa jana dhidi ya fc Basel |



Post a Comment