Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

SIMBA NA AZAM KATIKA MTIFUANO WA MAPINDUZI LEO USIKU




 Na. Imani Kelvin Mbaga, Dar es salaam

Timu za Simba na Azam za jijini Dar es salaam leo zinakutana katika mchezo wa fainali ya kombe la Mapinduzi, unaotarajiwa kuchezwa visiwani Zanzibar majira ya saa 2:15 usiku katika uwanja wa Aman

Fainali hiyo inachezwa baada ya Simba kuwaondoa wapinzani wao wa jadi, timu ya Yanga ya jijini Dar es salaam, katika mchezo wa nusu fainali yapili, kwa njia ya mikwaju ya penalt 4-2, huku katika nusu fainali ya kwanza Azam waliiondoa Taifa Jang’ombe kwa goli 1-0.

Mchezo wa leo unachezwa huku timu zote zikionekana kuwa kwenye kiwango bora hasa ukizingatia kuwa toka zilipoanza michuano hii hazijawahi kupoteza mchezo wowote.
Simba wanaonekana kuwa bora zaidi katika eneo la kiungo wakati mchezaji wao mpya James Kotei ameoneka kuwa bora kadri sik zinavyozidi kusonga, na kulifanya eneo la kiungo hasa cha kukaba kuonekana bora kwa klabu hiyo.

Azam wanaonekana kuwa bora zaidi katika eneo lao la ulinzi hususani ingizo jipya la Yakub Mohamed anaeonekana kuziba nafasi ya Pazcal Serge Wawa vyema katika eneo la ulinzi.

Bado timu zote zinaonekana kupata shida katika namna ya kutengenezana kuzitumia nafasi za kufunga katika michezo yao licha ya Azam kupata ushindi mnono katika mechi yao ya mwisho ya makundi dhidi yua timu ya Yanga kwa kuwaadhibu kwa magoli 4-0.

Pamoja na ushindi huo haiifanyi Azam kuwa bora katika safu yao ya ushambuliaji kwa hiyo bado kocha msaidizi wa wana lambalamba, Idd Nasor Cheche, ana kazi ya ziada leo hasa kwa kuwa atakuwa anakutana na safu bora ya ulinzi iliyo chini ya Mzimbabwe Method Mwanjali.

Kwa upande wa Simba pia bado washambuliaji wake hawajaonyesha cheche katika michuano yote na hadi hivi sasa viungo kama Muzamir Yassin na Mohamed Ibrahim “Mo” ndiyo wanaoonekana kuibeba timu yao katika ufungaji wa magoli jambo ambalo bado ni hatari kwa mechi kubwa kama ya leo.

Matarajio ya wachambuzi wengi wa soka ni kuona ufundi mkubwa katikati ya uwanja hasa kwa baadhi ya wachezaji wenye uwezo mkubwa wa kucheza na mpira na kuumiliki.
Vita kubwa kati ya Salum Aboubakar “sure boy”, Frank Domayo “chumvi”, kwa upande wa Azam na Jonas Mkude na James Kotei kwa upande wa Simba, ambao ndiyo uti wa mgongo wa kiungo kwa kila upande, bila shaka wao wataamua nini kifanyike na matokeo yatakuaje.

Baada ya mechi hiyo timu zote zitarudi Tanzania bara kuendelea na mtifuano wa ligi kuu, ambako Simba wanaongoza ligi hiyo wakifuatiwa na Yanga katika nafasi ya pili wakati Azam wanashika nafasi ya tatu.

No comments

Powered by Blogger.