TANZANIA YAIPANIA OLIMPIKI 2020 TOKYO JAPAN
| mkurugenzi wa michezo nchini, Omar Yusuph akitoa hotuba fupi wakati wa uzinduzi wa mpango wa kushiriki Olimpiki 2020 itakayofanyika Tokyo Japan |
Na Imani Kelvin Mbaga, Dar es salaam.
Shirikisho
la soka nchini Tanzania limezindua mpango mkakati utakaoiwezesha Tanzania
kupeleka timu ya mpira wa miguu kushiriki michuano ya Olimpiki 2020
inayotarajiwa kufanyika katika jiji la Tokyo nchini Japani.
Mgeni rasmi
ambaye ni mkurugenzi wa michezo nchini,
Omar Yusuph, kwa niaba ya serikali alisema wanaunga mkono jitihada
zinazofanywa na shirikisho la soka nchini katika kuhakikisha kuwa kuna
maendeleo yanayofikiwa katika soka.
“Serikali
inawapongeza sana, na inaahidi kuwaunga mkono katika kazi zenu, huku tukitanbua
kuwa katika mchezo wowote bila ya kuanza na vijana hatuwezi kupata maendeleo”
Alisema mkurugenzi huyo
Akizungumza
awali wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katika viwanja vya Karume jijini Dar
es salaam leo, Rais wa Shirikisho hilo, Jamal Malinzi, alisema mpango huu
unajumuisha timu za vijana wenye umri chini ya miaka 15, 17 na 19 ambao
wanafuzu kucheza michuano hiyo.
| Rais wa shirikisho la soka Tanzania (TFF) |
“Tunashukuru
kwamba tumefikia siku hii muhimu ambapo kama Watanzania wapenda soka
tunajumuika kushudia kuanza safari ya pamoja kuelekjea kutimiza ndoto zetu”
Alisema Malinzi
“Tumefanya
juhudi kubwa na tunaomba kungwa mkono na wadau wote kwani ni gharama kubwa
kuendesha mpira hasa soka la vijana, hata hivyo tumejizatiti ili kuhakikisha
kuwa ndoto zetu zinafanikiwa” Aliongeza.
Naye mshauri
wa soka la vijana nchini , Kim Polsen alisema kuwa mpira ni safari, na safari
siyo hatima bali ni mwendo unao taka moyo wa kupambana, na aliipongeza TFF kwa
kuanza safari hiyo kuelelekea Tokyo mwaka 2020
| Mshauri wa soka la vijana nchini Kim Poulsen |
“Nimefurahi
kuhudhuria uzinduzi huu muhimu sana kwa hatima ya soka la Tanzania, nimefurahi
pia kuwaona vijana wadogo ambo tumekuwa tukiwajenga kwa muda sasa ambao
ninaamini watakuja kuwa wakombozi wa soka letu” Alisema Polsen
Wageni
mbalimbali maarufu walikuwepo kwenye uzinduzi huo wakiwemo, Makamu wa Rais wa
kamati ya Olimpiki Tanzania, Henry Tandau, mwenyekiti wa soka la vijana ambaye
pia ni mwenyekiti wa chama cha mpira mkoa wa Dodoma, Mlamu Ng’ambi, kocha wa
timu ya taifa Salum Mayanga na wengine wengi.
| Katibu mkuu wa shirikisho la soka Tanzania, TFF, Selestine Mwesiga |
| Makamu wa Rais wa kamati ya Olimpiki Tanzania, Henry Tandau akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya ushiriki wa timu ya mpira wa miguu katika michuano ya Olimpiki 2020 Tokyo Japan |
| Mkurugenzi wa michezo nchini, Omar Yusuph akipiga mpira kuashiria uzinduzi wa kampeni ya kushiriki michuano ya Olimpiki 2020 Tokyo Japan |
| Viongozi, wachezaji na wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi wa kampeni ya kushiriki michuano ya Olimpiki 2020 wakiwa kwenye picha ya pamoja katika uwanja wa karume jijini Dar es salaam |
| vijana wa serengeti boys wakifanya mazoezi uwanja wa karume jijini Dr es salaam |
Post a Comment