ZIARA YA MSIMAMIZI WA CADESE KATIKA MRADI WA UMEME JUA WA MAJARIBIO, HOSPITALI YA WILAYA NYAMAGANA, MWANZA
Sehemu ya wodi za wagonjwa katika hospitali ya wilaya ya Nyamagana iliyofungwa umeme jua.
Mratibu wa Mradi wa Umeme Jua wa
Majaribio katika hospitali ya wilaya ya Nyamagana, Amin Abdallah,
(kulia) akielezea maendeleo ya mradi huo kwa Msimamizi wa Mradi wa
Kuwajengea Uwezo Wataalam wa Nishati na Tasnia ya Uziduaji (CADESE),
Paul Kiwele ( wa pili kutoka kulia). Wengine ni wataalam kutoka Sehemu
ya Nishati Jadidifu, Wizara ya Nishati na Madini.
Mratibu wa Mradi wa Umeme Jua wa
Majaribio katika hospitali ya wilaya ya Nyamagana, Amin Abdallah
(kulia) akieleza jambo kwa Mtaalam kutoka Sehemu ya Nishati Jadidifu-
Idara ya Nishati, Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Stephan
Kashushura (katikati). Kushoto ni Nasra Mohamed kutoka Wizara hiyo.
Mratibu wa Mradi wa Umeme Jua wa
Majaribio katika hospitali ya wilaya ya Nyamagana, Amin Abdallah
(kushoto mbele) akimwongoza Msimamizi wa Mradi wa Kuwajengea Uwezo
Wataalam wa Nishati na Tasnia ya Uziduaji (CADESE), Paul Kiwele (kulia
mbele) pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini katika
ziara kwenye mradi huo.
Mratibu wa Mradi wa Umeme Jua wa
Majaribio katika hospitali ya wilaya ya Nyamagana, Amin Abdallah
(kulia) akielezea mfumo wa kuongozea vifaa vya umeme jua katika
hospitali ya wilaya ya Nyamagana.
Mratibu wa Mradi wa Umeme Jua wa
Majaribio katika hospitali ya wilaya ya Nyamagana, Amin Abdallah
(kushoto) akionesha mita maalum ya kuruhusu umeme kuingia na kutoka
kwenye Gridi ya Taifa.
Mratibu wa Mradi wa Umeme Jua wa
Majaribio katika hospitali ya wilaya ya Nyamagana, Amin Abdallah ( wa
pili kutoka kulia) akionesha karabai zinazotumia umeme jua zilizotolewa
na mradi huo kwa wavuvi wa soko la samaki la Mwaloni jijini Mwanza.
Mmoja wa wavuvi katika soko la
samaki la Mwaloni jijini Mwanza, Joseph Athony (kushoto) akielezea
manufaa ya karabai zinazotumia umeme jua zilizotolewa na Mradi wa Umeme
Jua wa Majaribio.
Post a Comment