Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

SAMATTA KUTUA KUWAKABILI ZIMBABWE



Na: Imani Kelvin Mbaga


Mbwana Samatta nahodha wa Taifa Stars
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anaechezea klabu ya Genk ya nchini Ubelgiji, Mbwana Ally Samatta, anatarajiwa kuwasili leo saa sita usiku kujiunga na kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, kilichoweka kambi katika hoteli ya Urban Rose jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Zimbabwe inayotarajiwa kuchezwa mwishoni mwa juma hili.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaji wa shirikisho la soka nchini Alfred Lucas, ilisema kuwa, mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Tanzania atakuja kuungana na wenzake ili kujiandaa na mechi hiyo muhimu kwa lengo la kupata ushindi ili kuinua viwango vya timu ya taifa katika msimamo wa ubora unaotolewa kila mwezi na shirikisho la soka la kimataifa, FIFA.
Wachezaji wengine walioitwa na kocha mkuu wa timu hiyo, Charles Boniface Mkwasa ni

Makipa
Deogratius Munishi             –Young Africans
Said Kipao                        –JKT Ruvu
Aishi Manula                     –Azam FC
Mabeki
Erasto Nyoni                     -Azam FC
Michael Aidan                    -JKT Ruvu
Mwinyi Haji                      -Young Africans
Mohamed Hussein              –Simba SC
David Mwantika                 -Azam FC
James Josephat                 –Tanzania Prisons
Vicent Andrew                   -Young Africans
Viungo wa Kati
Himid Mao                        -Azam FC
Mohammed Ibrahim            –Simba SC
Jonas Mkude                     –Simba SC
Muzamiru Yassin                –Simba SC
Viungo wa Pembeni
Abdulrahman Mussa            -Ruvu Shooting        
Shiza Kichuy                      –Simba SC
Simon Msuva                     -Young Africans
Jamal Mnyate                    –Simba
Washambuliaji
Ibrahim Ajib                      –Simba SC
John Bocco                        -Azam FC
Mbwana Samatta                -K.R.C Genk ya Ubelgiji
Elius Maguli                       –Oman
Thomas Ulimwengu            –Mchezaji huru
Omar Mponda                    -Ndanda
Hii itakuwa ni mechi muhimu sana kwa timu ya taifa kutokana na nafasi iliyopo katika msimamo wa ubora duniani kwa mujibu wa FIFA

No comments

Powered by Blogger.