Your Business Looks Here

Your Business Looks Here
tupo kwenye tathimini ya mwaka radio itarudi hewani kuanzia tarehe 25

TWIGA KAMILI YAIFUATA CAMEROON



Kikosi cha timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars

Na: Imani Kelvin Mbaga

Kikosi cha wachezaji 17 na viongozi wanne cha timu ya taifa ya wanawake Tanzania, Twiga Stars, kimeondoka leo kwenda nchini Cameroon kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa na timu ya taifa ya wanawake ya nchi hiyo kufuatia mwaliko waliopata kutoka shikirisho la soka la  Cameroon, FECAFOOT.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo msemaji wa shirikisho la soka la Tanzania, Alfred Lucas, alisema timu hiyo inatarajiwa kutua jijini Younde baadae leo na kwamba kikosi cha wachezaji hao 17 kitakuwa huko kuliwakilisha taifa pamoja na kupata kipimo halisi kujiandaa na michuano mbalimbali.
Hata hivyo Lucas alisema wachezaji 20 waliitwa tayari kwa ajili ya mechi hiyo lakini wachezaji watatu kati yao wameshindwa kusafiri na timu kwa sababu mbalimbali ikiwemo majeruhi na kuchelewa kwa visa.
“Mwalimu aliita wachezaji 20 wa timu yetu ya Twiga Stars, lakini kwa bahati mbaya wachezaji 17 pekee ndiyo wameondoka na timu hiyo kwa sababu mbalimbali ikiwemo kuchelewa kwa viza, hata hivyo kwa kuwa ni mchezo mmoja tu wa kirafiki, kukosekana kwao hakutaathiri kikosi kwa jumla” Alisema Lucas.
Msemaji huyo aliwataja wachezaji hao kuwa ni
Walinda mlango:
Fatma Omary
Najiat Abas
Walinzi
Wema Richard
Sophia Mwasikili (nahodha)
Anastazia Katunzi
Fatma Issa
Maimuna Hamiss
Happiness Mwaipaja
Marry Massatu
Viungo
Donisia Minja
Amina Ally
Situmai Abdallah
Anna Mwaisula
Fadhila Kigalawa
Washambuliaji
Fatma Swaleh
Asha Rashid “Mwalala”
Mwanahamisi Omary
Viongozi waliosafiri na timu hiyo ni pamoja na
Sebastian Nkoma (kocha mkuu)
Edna Lema(kocha msaidizi)
Eliutel Mollel
Wakati ambapo mwenyekiti wa soka la wanawake Amina Kaluma anatarajia kuondoka kesho kujiunga na timu hiyo.

No comments

Powered by Blogger.